KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, July 23, 2014

VODACOM KUDHAMINI ZIARA YA ZIARA YA REAL MADRID


VODACOM Tanzania ni miongoni mwa makampuni yaliyojitokeza kudhamini ziara kikosi cha wachezaji nyota waliowahi kutamba Real Madrid ya Hispania, maarufu kama Real Madird Legends ambao watazuru nchini mwezi ujao.


Meneja ziara ya magwiji wa Real Madrid, Dennis Ssebo amewaambia Waandishi wa Habari asubuhi ya leo katika hoteli ya New Africa, Dar es Salaam kwamba, mbali na Vodacom, wadhamini wengine wa ziara hiyo ni Fastjet, Tropical, Pembe Flower, Lake Gas, EFM Radio na Ladger Plaza Bahari Beach.

Wachezaji waliotamba kuanzia La Liga, wakacheza ligi nyingine za Ulaya, Kombe la Ulaya, Ligi ya Mabingwa na Kombe la Dunia waliowahi kuchezea Madrid watakuja nchini Agosti 22.

Katika ziara hiyo, pamoja na kucheza mchezo wa kirafiki na kikosi maalum cha wachezaji nyota wa Tanzania, pia watafanya utalii katika vivutio mbalimbali, ikiwemo kupanda mlima Kilimanjaro.

Real Madrid inakuja nchini kwa mwaliko wa kampuni ya Tanzania Sisi ni Nyumbani (TSN), chini ya Mkurugenzi wake Mkuu, Farough Baghozah.

Miongoni mwa nyota wanaotarajiwa kuja na Real nchini ni pamoja na Wanasoka Bora wa zamani wa Dunia, Mfaransa Zinadine Zidane, Mreno Luis Figo na Mbrazil, Ronaldo Lima.

Magwiji hao wa Real tayari wamekwishafanya matangazo ya ziara yao nchini wakisema wana hamu mno ya kukanyaga ardhi ya Tanzania.

No comments:

Post a Comment