KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, July 9, 2014

KIINGILIO STARS, MSUMBIJI BUKU SABA


KIINGILIO cha chini cha mechi kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Msumbiji (Mambas)
itakayochezwa Julai 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kitakuwa sh. 7,000.

Tiketi zinapatikana kwa mfumo wa elektroniki kupitia M-PESA. Kiingilio hicho kwa ajili
ya viti vya rangi ya rangi ya chungwa, kijani na bluu. Viingilio katika maeneo mengine
vitatangazwa baadaye.

Mshabiki ili apate tiketi anatakiwa kutumia M-PESA kwa kupiga *150*00# kisha
bonyeza 4, ingiza namba ya kampuni 173399 kisha weka 7000 kwenye namba ya
kumbukumbu ya malipo, na weka 7000 kama kiasi cha bei ya tiketi na mwisho weka
namba yao ya siri.

Baada ya hapo utapokea ujumbe wenye orodha ya vituo vya MaxMalipo kwa ajili ya
kuchukulia tiketi ukiwa na namba ya uhakiki wa malipo yako.

Vituo vya kuchukulia tiketi ni mgahawa wa Steers uliopo mtaa wa Samora/Ohio, maduka
makubwa ya Uchumi Supermarket (Quality Centre, Tabata Segerea na kituo cha
daladala Makumbusho), Sheer Illutions (Millennium Tower na Mlimani City), maduka
makubwa ya TSN Supermarket (City Centre, Kibo Tegeta na Upanga).

Vodashop (Ubungo na Mill Pamba), Shop Mwenge (Born to Shine), Puma Petrol
Station (Mwenge na Uwanja wa Ndege), Engen Petrol Station (Mbezi Beach), Big Bon
Petrol Station (Kariakoo, Sinza Mori, Mbagala na Temeke), YMCA (Posta Mpya), City
Sports Lounge (Posta), Uwanja wa Taifa) na ofisi za TFF (PPF Tower).

No comments:

Post a Comment