KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, July 8, 2014

WASANII WA TANZANIA WATIA FORA KWA MUZIKI WA KIASILI UJERUMANI


Muziki wa dansi wa Tanzania umezidi kufungua ukurusa mpya katka tufe la dunia,
baada ya wasanii na wanamuziki wa Tanzania kutumbuiza katika onyesho la TFF Rudolstadt 2014,yaliofanyika kuanzia tarehe 3 adi 6 Julai 2014 mjini Rudolstadt,Ujerumani,ambako vikundi mbali mbali vya sanaa na bendi za muziki kutoka Tanzania zilishiriki,zikiwemo bendi ya Black Warriors ikiwashirikisha jukwaani na wakongwe wa muziki akina Mafumu Bilal,Hassan Bichuka,Cosmas Chidumule na wengine,pia Mchiriku ulikuwapo,bila kukosa Kikundi cha ngoma ya Kaya Baikoko
kutoka mkoani Tanga, kikundi cha Qwasida " Tarbiyya Islamiyya" kutoka Zanzibar, Kikundi cha kinamama cha Ngoma za Wagogo kutoka Dodoma, Mambo moto moto band na Segere lao walikuwapo hayo yote yalikuwa mjini Rudolstad, nchini Ujerumani nchi ambayo ndipo makao makuu ya "FFU-Ughaibuni"

WASANII wa kundi la muziki la Segere Orijino wakifanya vitu vyao 
MWIMBAJI wa muziki wa Baikoko kutoka Tanga akiwajibika

MPULIZA saxaphone maarufu nchini, Mafumu Bilali 'Bombenga' akionyesha umahiri wake
HILI ni kundi zima la Black Warriors likiongozwa na Cosmas Chidumule na Hassan Bitchuka

 HASSAN Bitchuka na Cosmas Chidumule wakifanya vitu vyao
SEHEMU ya umati wa watu waliohudhuria onyesho hilo

No comments:

Post a Comment