KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, July 19, 2014

SIMBA KUJIPIMA UBAVU NA ISMAILI TAMASHA LA SIMBA DAY



SIMBA SC itacheza na Ismailia ya Misri au Zesco United ya Zambia katika tamasha maalum la klabu hiyo la kila mwaka, maarufu kama Simba Day Agosti 9, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Makamu wa Rais wa Simba SC, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ amesema leo katika mkutano na Waandishi wa Habari makao makuu ya klabu, Mtaa wa Msimbazi kwamba, kipaumbele cha kwanza ni Ismailia na iwapo itashindikana Zesco itachukua nafasi.

Kaburu amesema mchakato wa usajili unaendelea na jana mchezaji wa Burundi amewasili wakati kesho Kamati ya Usajili itakutana naye kwa mazungumzo.

Simba SC inaendelea na mazoezi Dar es Salaam
Beki Mrundi, Kaze Gilbert ameomba aandikiwe barua ya ruhusa ya kwenda kujiunga na klabu yake ya zamani, Vital’O, wakati beki chipukizi Hassan Hatibu anatakiwa na Kagera Sugar.

Kaburu amesema wamekubali maombi yote la Kaze na Kagera Sugar na watawaidhinishia wachezaji hao, ambao kwa sasa hawana nafasi kwenye kikosi cha Wekundu hao wa Msimbazi.

Amesema klabu hiyo pia imeridhia mshambuliaji wake Betram Mombeki kujiunga na JKT Ruvu, maana yake imefuta mkataba wake.

Kuhusu kocha wa timu hiyo, Mcroatia Zdravko Logarusic aliyemaliza Mkataba wake, Kaburu amesema kwamba wanatarajia kumpa Mkataba mpya wiki ijayo kabla ya timu kwenda kambini visiwani Zanzibar kujiandaa na msimu mpya.

Simba SC pia imetangaza nafasi za kazi kwa Katibu, Msaidizi wake na Ofisa Habari na Kaburu ameomba watu watume maombi ili kuiwezesha klabu kufanya uteuzi. Katibu wa Simba SC kwa sasa ni Ezekiel Kamwaga, wakati Ofisa Habari ni Asha Muhaji

IMETOLEWA KUTOKA BLOGU YA BIN ZUBEIRY

No comments:

Post a Comment