KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, July 9, 2014

TAIFA STARS YAINGIA KAMBINI TUKUYU


Wakati Taifa Stars inaingia kambini Tukuyu mkoani Mbeya kesho (Julai 9 mwaka huu),
kocha Mart Nooij amesema kambi ya wiki mbili nchini Botswana imekisaidia kikosi
chake kujiandaa kwa ajili ya mechi dhidi ya Msumbiji.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo (Julai 8 mwaka huu) kuhusu maandalizi ya timu
hiyo, Nooij amesema timu yake inafanya mazoezi kwenye maeneo ya baridi kwa sababu
za kitaalamu, hivyo kambi ya Tukuyu kama ilivyokuwa ya Botswana itawasaidia kwa
mechi dhidi ya Msumbiji.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itaondoka kwa ndege
kwenda Mbeya ikiwa na kikosi cha wachezaji 25, na itarejea jijini Dar es Salaam siku tatu
kabla ya mechi hiyo.

Wachezaji walioko kwenye msafara huo ni Aggrey Morris, Aishi Manula, Amri Kiemba,
Benedictor Tinoko, Deogratius Munishi, Edward Charles, Emmanuel Namwando,
Erasto Nyoni, Haruni Chanongo, Himid Mao, John Bocco na Jonas Mkude.

Wengine ni Joram Mgeveke, Kelvin Friday, Kelvin Yondani, Khamis Mcha, Mrisho
Ngasa, Mwagane Yeya, Nadir Haroub, Oscar Joshua, Pato Ngonyani, Ramadhan
Singano, Said Juma, Said Moradi, Shabani Nditi, Shomari Kapombe, Simon Msuva,

Mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya kutafuta tiketi ya kucheza fainali za
Afrika (AFCON) dhidi ya Msumbiji itafanyika Julai 20 mwaka huu kwenye Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment