KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, July 23, 2014

LOGA AMWAGA WINO SIMBA MIAKA MIWILI


KOCHA Mkuu wa Simba SC, Mcroatia Zdravko Logarusic amesaini Mkataba mpya wa mwaka mmoja na kusema kwamba timu hiyo itakuwa bora msimu ujao, ubingwa wa Ligi Kuu ikiwa lengo la kwanza.


Akizungumza makao makuu ya klabu, Mtaa wa Msimbazi baada ya kusaini Mkataba huo, kocha huyo wa zamani wa Gor Mahia ya Kenya amesema kwamba amefurahi kusaini kandarasi mpya na sasa anaelekeza nguvu zake kwenye kazi.

Loga amesema Simba SC itakuwa timu bora msimu ujao na lengo lake kuu ni kuhakikisha inatwaa ubingwa.

Kwa upande wake, Makamu wa Rais Simba, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ aliyesaini Mkataba na kocha huyo amesema kwamba sasa msalaba mkubwa wa Loga ni kuhakikisa Kombe la ubingwa wa Ligi Kuu msimu ujao linatua Msimbazi.

Kaburu pia amesema Kocha Msadizi, Suleiman Matola ‘Bin Laden’ naye alisaini Mkataba wa miaka miwili tangu Novemba mwaka jana.

Loga alijiunga na Simba SC Desemba mwaka jana kwa Mkataba wa miezi sita, lakini uongozi wa klabu hiyo umeridhishwa na kazi yake na kumuongeza mwaka mmoja mwingine.

No comments:

Post a Comment