KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, July 18, 2014

FIFA KUWANOA WAAMUZI 30 DAR



Semina na mtihani wa utimamu wa mwili (physical fitness test) kwa waamuzi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) na baadhi ya wale wa daraja la kwanza wenye kiwango cha juu (elite) itafanyika jijini Dar es Salaam.

Waamuzi 30 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar watashiriki kwenye semina hiyo itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia Julai 21 hadi 26 mwaka huu.

Mkufunzi wa FIFA kwa Kanda ya Kusini mwa Afrika, Carlos Henriques kutoka Afrika Kusini ndiye atakayeendesha semina hiyo akisaidiwa na Watanzania Charles Mchau kutoka Kilimanjaro, Juma Ali David (Zanzibar), Joan Minja (Dar es Salaam) na Riziki Majala (Pwani).

Waamuzi na waamuzi wasaidizi wa FIFA watakaoshiriki semina hiyo ni Ferdinand Chacha (Mwanza), Hamisi Chang’walu (Dar es Salaam), Israel Mujuni (Dar es Salaam), Jesse Erasmo (Morogoro), John Kanyenye (Mbeya), Josephat Bulali (Zanzibar), Kinduli Ali (Zanzibar), Oden Mbaga (Dar es Salaam), Ramadhan Ibada (Zanzibar), Samwel Mpenzu (Arusha) na Waziri Sheha (Zanzibar).

Kwa upande wa waamuzi wa daraja la kwanza ni Abdallah Kambuzi (Shinyanga), Agnes Pandaleo (Arusha), Ahamada Simba (Kagera), Arnold Bugado (Singida), Charles Simon (Dodoma), Dalila Jafari (Zanzibar), Frank Komba (Pwani), Helen Mduma (Dar es Salaam), Issa Bilali (Zanzibar) na Issa Haji (Zanzibar).

Wengine ni Janeth Balama (Iringa), Jonesia Rukyaa (Kagera), Lulu Mushi (Dar es Salaam), Martin Saanya (Morogoro), Mary Kapinga (Ruvuma), Mbaraka Haule (Zanzibar), Mfaume Ally (Zanzibar), Mohamed Mkono (Tanga) na Soud Lila (Dar es Salaam).

Washiriki wa semina hiyo na wakufunzi wanatakiwa kuwasili jijini Dar es Salaam, Julai 20 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment