KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, July 18, 2014

MBRAZIL MWINGINE ATUA YANGA


Mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Brazil Geilson Santos Santana "Jaja" amewasili

leo mchana jijini Dar es salaam akitokea jijini Sao Paul tayari kwa kuanza kazi ya
kuitumikia klabu ya Young Africans Sports Club kwa msimu wa 2014/2015.

Jaja ambaye alikua akichezea timu ya Itabaina FC nchini Brazil, anakuwa ni mchezaji wa
pili kuungana na kikosi cha Young Africans baada ya Andrey Coutinho kuwa mchezaji
wa kwanza kujiunga na kikosi cha kocha Marcio Maximo.

Usajili wa wachezaji hawa ni muendelezo wa uongozi wa Young Africans kuhakikisha
msimu ujao unakua na kikosi bora ambacho kitaweza kufanya vizuri kwenye michuano
ya Ligi Kuu ya Vodacom na mashindano ya Kombe la Shrikisho Barani Afrika.

Jaja anaungana na makocha wabrazil Marcio Maximo na Leonardo Neiva na kiungo
Andrey Coutinho katikaa msimu huu ambapo kwa pamoja ushirikiano wao na wachezaji
wengine wazawa wataisaidia Young Africans kufanya vizuri.

Kesho asubuhi Jaja anatarajiwa kuanza mazoezi katika shule ya sekondari Loyola ikiwa
ni sehemu ya maandaliz ya michuano mbalimbali itayowakabili

No comments:

Post a Comment