KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, July 31, 2014

AZAM ACADEMY BINGWA KOMBE LA ROLLINGSTONE



AZAM FC imetwaa ubingwa wa michuano ya vijana chini ya umri wa miaka 20 kwa nchi za Maziwa Makuu, maarufu kama Rollingston baada ya kuichapa timu ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) ya Mgulani Twalipo bao 2-0 katika fainali jioni hii Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

Jamil Mchaulu ‘Balotelli’ aliyefunga bao la kwanza dakika ya tatu, baada ya kuwatoka vizuri beki wa kulia wa Twalipo, Ally Mbonde na beki wa kati Ally Athumani kisha kumtungua kipa wao, Kulwa Baumba.


Twalipo ilipoteza mwelekeo mapema tu baada ya bao hilo, na wachezaji wake kuanza kucheza rafu nyingi, badala ya kutengeneza mipangop ya kusawazisha bao.

Azam walitumia mwanya huo kucheza mpira wa kuachiana pasi za haraka uwanjani kuwakwepa ‘wapiga kiatu’ wa jeshini na kufanikiwa kumaliza dakika 45 za kwanza wakiwa wanaongoza 1-0.

Kipindi cha pili, mchezo ulizidi kunoga, Twalipo wakisaka bao la kusawazisha na Azam wakitafuta mabao zaidi- hali iliyosababisha mashambulizi ya pande zote mbili.

Alikuwa ni Adam Omar Soba aliyeihakikishia Kombe la kwanza la Rollingston Azam FC baada ya kufunga bao la pili dakika ya 88.

Katika mchezo wa kwanza wa kuwsaka mshindi wa tatu, Champion ya Kawe ilitwaa ubingwa wa U17 kwa kuifunga Bom Bom ya Ilala kwenye Uwanja huo huo, Karume.

No comments:

Post a Comment