KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, July 21, 2014

TAIFA STARS YABANWA MBAVU NA MSUMBIJI



MSHAMBULIAJI Thomas Ulimwengu wa Taifa Stars akimtoka beki wa Msumbiji jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
MSHAMBULIAJI Mbwana Samatta wa Taifa Stars akiwafungisha tela mabeki wa Msumbiji
KIPA Deogratius Munishi 'Dida' wa Taifa Stars akishangilia bao la pili la timu hiyo kwa kuonyesha maandishi kwenye fulana yake.

TIMU ya soka ya Taifa, Taifa Stars jana ililazimishwa kutoka sare ya mabao 2-2 na Msumbiji katika mechi ya michuano ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Afrika iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Sare hiyo imeiweka Taifa Stars katika mazingira magumu ya kusonga mbele kwa vile italazimika kushinda mechi ya marudiano mjini Maputo kwa idadi yoyote ya mabao ama kuomba ipate sare ya mabao zaidi ya matatu.

Taifa Stars, inayofundishwa na Kocha Mart Nooj kutoka Uholanzi, ilicheza soka ya kuvutia kipindi cha kwanza na kufanya mashambulizi mengi kwenye lango la Msumbiji.

Msumbiji ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 47 lililofungwa na Elias Pelembe kwa mkwaju wa penalti baada ya beki Kevin Yondan kumchezea vibaya Helder Pelembe ndani ya eneo la hatari.

Kiungo wa Taifa Stars, Mcha Khamis aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Mrisho Ngasa, alifunga bao la kusawazisha dakika ya 60, akiunganisha mpira wa krosi uliopigwa na Thomas Ulimwengu.

Mcha aliwainua tena vitini mashabiki dakika ya 71 baada ya kuifungia Taifa Stars bao la pili kwa njia ya penalti baada ya Samatta kuangushwa ndani ya eneo la hatari.

Zikiwa zimesalia dakika tatu pambano hilo kumalizika, Isac de Carvalho aliisawazishia Msumbiji kutokana na uzembe wa mabeki wa Taifa Stars.

No comments:

Post a Comment