KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, July 23, 2014

YANGA KUFUNGUA DIMBA NA RAYON KOMBE LA KAGAME


YANGA imepangwa kufungua dimba la michuano ya soka ya Kombe la Kagame kwa kumenyana na wenyeji, Rayon Sports kwenye dimba la Amahoro mjini Kigali.


Ratiba ya michuano hiyo iliyotolewa juzi na Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), inaonyesha kuwa mechi hiyo itapigwa Agosti 8 mwaka huu.

Wawakilishi hao wa Tanzania Bara wamepangwa kundi A pamoja na timu za Rayon, Coffee ya Ethiopia, Atlabara ya Sudan Kusini na KMKM ya Zanzibar.

Kundi B litakuwa na timu za APR ya Rwanda, KCC ya Uganda, Flambeau Del Est ya Burundi, Telecom ya Djibouti na Gor Mahia ya Kenya.

Timu zilizopangwa kundi C ni Vital'O ya Burundi, El Merreikh ya Sudan, Police ya Rwanda na Banadir ya Ethiopia.

Kwa mujibu wa ratiba, mbali na mechi ya ufunguzi kati ya Yanga na Rayon, mechi zingine za ufunguzi zitazikutanisha Atlabara na KMKM na kati ya Gor Mahia na KCC.

No comments:

Post a Comment