KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, July 23, 2014

JAMES RODRIGUEZ ATAMBULISHWA RASMI REAL MADRID




 
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Colombia, James Rodriguez, juzi alitambulishwa rasmi na klabu yake mpya ya Real Madrid ya Hispania.

James amemwaga wino wa kuichezea Real Madrid kwa miaka sita na uhamisho wake umeigharimu klabu hiyo pauni milioni 60 za Uingereza na kuwa mchezaji ghali wa nne duniani.

Maelfu ya mashabiki wa Real Madrid walifurika kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu wakati nyota huyo wa Kombe la Dunia alipokuwa akitambulishwa na Rais wa klabu hiyo, Florentino Perez.

Utambulisho huo uliingia doa baada ya shabiki mmoja, anayesadikiwa kuwa ni kutoka Colombia, alipovamia ndani ya uwanja na kwenda moja kwa moja kumkumbatia James kabla ya kutolewa na polisi.

Rekodi ya mchezaji ghali duniani kwa sasa inashikiliwa na Gareth Bale, ambaye uhamisho wake uliigharimu Real Madrid pauni milioni 80, akifuatiwa na Cristiano Ronaldo, aliyenunuliwa pia kwa pauni milioni 80. Luis Suarez anashika nafasi ya tatu kutokana na uhamisho wake kuigharimu Barcelona pauni milioni 75.

Real Madrid imemuhamisha James kutoka Monaco ya Ufaransa. Wakati wa utambulisho wake, Perez alimpeleka mchezaji huyo kwa nyota wa zamani wa klabu hiyo, Alfredo Di Stefano, ambaye pia alihamishwa kutoka Colombia.

WACHEZAJI 10 GHALI DUNIANI
£80m - Gareth Bale (Tottenham to Real Madrid)
£80m - Cristiano Ronaldo (Manchester United to Real Madrid)
£75m - Luis Suarez (Liverpool to Barcelona)
£60m - James Rodriguez (Monaco to Real Madrid)
£59m - Zlatan Ibrahimovic (Inter Milan to Barcelona)
£56m - Kaka (AC Milan to Real Madrid)
£55m - Edinson Cavani (Napoli to PSG)
£51m - Radamel Falcao (Atletico Madrid to Monaco)
£50m - Fernando Torres (Liverpool to Chelsea)
£50m - David Luiz (Chelsea to PSG)

No comments:

Post a Comment