KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, May 23, 2013

MESSI: HATUPASWI KUBADILI STAILI YETU YA UCHEZAJI



MADRID, Hispania
MWANASOKA bora wa dunia, Lionel Messi ameitaka klabu yake ya Barcelona ya Hispania isibadili staili yake ya uchezaji.

Messi alisema mjini hapa juzi kuwa, wanapaswa kuendelea na staili hiyo licha ya kushindwa kufika mbali katika michuano ya ligi ya mabingwa wa Ulaya msimu.

Barcelona ilitolewa katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo baada ya kupata kipigo cha jumla cha mabao 7-0 kutoka kwa Bayern Munich ya Ujerumani.

Kutolewa mapema kwa Barcelona katika michuano hiyo, kumetafsiriwa kuwa, kumetokana na staili ya uchezaji ya timu hiyo kuzidiwa na ile ya Bayern Munich.

"Hatuwezi kupoteza vichwa vyetu. Hatuwezi kubadili staili yetu ya uchezaji," alisema mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 25.

"Huwezi kushinda siku zote. Tumekuwa tukicheza kwa kiwango cha juu kwa miaka kadhaa na makocha na timu zingine zimekuwa zikijifunza kutoka kwetu,"aliongeza mchezaji huyo.

Messi alisema wanapaswa kuwa watulivu na kujipanga upya kwa ajili ya michuano ya msimu ujao.

Makamu wa rais wa klabu hiyo, Josep Bartomeu alisema wanapaswa kuongeza wachezaji wapya wanne au watano kwa ajili ya kukiimarisha kikosi chao.

No comments:

Post a Comment