KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, May 23, 2013

SUAREZ AZUA HOFU LIVERPOOL



LONDON, England
KOCHA Mkuu wa Liverpool, Brendan Rodgers amekiri kuwa, anatarajia kukumbana na upinzani mkali katika kumzuia mshambuliaji, Luis Suarez asiondoke.

Rodgers alisema juzi mjini hapa kuwa, licha ya Liverpool kumuunga mkono mchezaji huyo wa kimataifa wa Uruguay, hali inaweza kubadilika iwapo ataamua kuondoka.

Wakati Rodgers alipokabidhiwa kibarua cha kuinoa timu hiyo msimu uliopita, jukumu lake la kwanza lilikuwa ni kuzikataa ofa kutoka klabu za Juventus ya Italia na Paris St Germain za kutaka kumsajili mchezaji huyo.

Suarez ametia saini mkataba mpya wa kuichezea Liverpool hadi 2017, lakini mustakabali wake katika klabu hiyo bado una utata.

Mshambuliaji huyo kutoka Uruguay alimaliza msimu uliopita kwa matatizo, ikiwa ni pamoja na kufungiwa mechi 10 kwa kumng'ata beki Branislav Ivanovic wa Chelsea.

Hadi sasa, mchezaji huyo ameshatumikia adhabu hiyo katika mechi nne na amekabisha mechi sita, ambazo atazitumikia msimu ujao.

Klabu ya Juventus imeshaonyesha tena nia ya kumsajili mshambuliaji huyo, ikiwemo Atletico Madrid ya Hispania. Suarez pia amekuwa akihusishwa na mipango ya kujiunga na Bayern Munich ya Ujerumani.

"Sina wasiwasi wa kupokea ofa kutoka klabu zingine kwa sababu yupo kwenye kiwango cha juu,"alisema Rodgers.

"Kuna asilimia chache ya wachezaji walioko kwenye kiwango cha dunia. Suarez yumo kwenye orodha hiyo. Lazima kuna klabu zitamuhitaji,"aliongeza.

Hata hivyo, Rodgers alijipa moyo kwa kusema kuwa, ana hakika Suarez anapenda kubaki katika klabu hiyo kwa vile anafurahia kucheza soka England.

No comments:

Post a Comment