KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, May 16, 2013

KIEMBA, CHOLO, KAZIMOTO WATEMWA TAIFA STARS


KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa 'Taifa Stars' Kim Poulsen, amewaacha wachezaji watano katika kikosi chake kitakachoingia kambini kujiwinda na mchezo dhidi ya Morocco.


Wachezaji hao na timu wanazotoka ni Issa Rashid na Shaaban Nditi (Mtibwa Sugar), Nassor Masoud ‘Chollo’, Mwinyi Kazimoto na Amri Kiemba (Simba).

Katika timu hiyo, Poulsen amemuita kipa wa Yanga Ally Mustafa 'Bartez' na Zahor Pazi wa JKT Ruvu ambao walikuwa nje ya timu hiyo kwa muda.

Poulsen alisema wachezaji hao wataingia kambini Mei 20 kujiwinda na mchezo dhidi ya Morocco huku pia wakijiandaa na mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Sudan.

Kocha huyo alisema timu yake itacheza na Sudai Juni 2 mwaka huu kabla ya kwenda Morocco na kusema mchezo huo ni muhimu kwa ajili ya kuimarisha kikosi chake.

Alisema tayari programu ya kambi ya timu hiyo imekwishaandaliwa na ni matarajio yake kuwa timu itajiandaa vyema na kufanikisha malengo yake.

Stars iliyopo kundi C na timu za Ivory Coast, Morocco na Gambia inashika nafasi ya pili katika kundi hilo ikiwa na pointi sita nyuma ya Ivory Coast yenye pointi saba.

Kikosi kamili cha timu hiyo kinaundwa na makipa Ally Mustafa ‘Barthez’ (Yanga), Juma Kaseja wa (Simba), Mwadini Ally na Aishi Manula (Azam).

Mabeki ni Erasto Nyoni, Aggrey Morris (Azam), Kevin Yondan, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ (Yanga), Shomary Kapombe (Simba), na Yahya Mudathir (Azam).

Viungo ni Haroun Chanongo na Mrisho Ngassa (Simba), Simon Msuva, Frank Domayo na Athumani Iddi ‘Chuji’ (Yanga), Salum Abubakar, Vicent Barnabas, Khamis Mcha ‘Vialli’ (Azam) wakati washambuliaji ni Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu (TP Mazembe), John Bocco(Azam FC), Juma Luizio (Mtibwa Sugar) na Zahor Pazi (JKT Ruvu).

No comments:

Post a Comment