KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, May 1, 2013

JAYDEE KUZINDUA ALBAMU MPYA MEI 31

MWANAMUZIKI mkongwe nchini, Judith Wambura 'Lady JayDee' anatarajia kuzindua albamu yake mpya katika onyesho litakalofanyika Mei 31 mwaka huu.

Akizungumza mjini Dar es Salaam wiki hii, Lady JayDee alisema albamu yake hiyo yenye nyimbo 10, ambayo ni ya sita, itajulikana kwa jina la Nothing but the truth.

JayDee alisema onyesho hilo litafanyika kwenye ukumbi wa Nyumbani Lounge uliopo Msasani, Dar es Salaam.

Alisema uzinduzi wa albamu hiyo utakwenda sambamba na sherehe za kutimiza kwake miaka 13 tangu alipojitosa kwenye fani ya muziki.

"Nawashukuru sana mashabiki wangu kwa kuendelea kuniunga mkono na kunipa nguvu. Pia navidhukuru vyombo vya habari kwa kukuza na kuilinda sanaa ya Tanzania bila kujali maslahi binafsi,"alisema msanii huyo, ambaye anamiliki bendi ya Machozi.

Kwa mujibu wa JayDee, katika onyesho hilo, atapiga nyimbo zake zote zilizowahi kutamba, ikiwa ni pamoja na zile alizowashirikisha wasanii mbalimbali nchini.

Alisema onyesho la uzinduzi wa albamu hiyo litadhaminiwa na kituo cha televisheni cha East Africa

No comments:

Post a Comment