KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, December 13, 2016

SIMBA HOI KWA MTIBWA SUGAR



MTIBWA Sugar imepata ushindi wa kufungia mwaka dhidi ya Simba SC, baada ya kuichapa mabao 2-1  jioni ya leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Kocha Mcameroon, Joseph Marius Omog aliwaanzisha Waghana wote, kipa Daniel Agyei na kiungo James Kotei, lakini wakashindwa kuwafurahisha mashabiki wa timu hiyo.
Mtibwa Sugar ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao dakika ya kwanza tu ya mchezo huo, mfungaji Stahmili Mbonde aliyefumua shuti kali lililompoita kipa mpya kutoka Ghana, Daniel Agyei baada ya kufanikiwa kuwapiga chenga mabeki wa Simba.
Simba ilicharuka na kupeleka mashambulizi mengi langoni mwa Mtibwa Sugar kutaka kusawaziha, hata hivyo safu ya ulinzi ya Wakata Miwa wa Manungu iliyokuwa ikiongozwa na Salim Mbonde ilisimama imara kuzuia hatari zote.
 Mtibwa Sugar ikafanikiwa kupata bao la pili dakika ya 34 mfungaji Jaffari Salum aliyewapiga chenga mabeki wa Simba baada ya kupokea pasi nzuri ya Ally Shomary na kumchambua Agyei tena.
Dakika mbili baadae Simba wakapata bao, dakika ya 36 lililofungwa na kiungo wa zamani wa Mtibwa, Mohamed ‘Mo’ Ibrahim kwa shuti la kushitukiza lililompita kwa urahisi, kipa Said Mohammed aliyekuw amezubaa.
Kipindi cha pili, Simba iliongeza kasi ya mashambulizi langoni mwa Mtibwa, lakini bado wapinzani wao hao waliendelea kuwa makini katika kujilinda.
Beki Janvier Besala Bokungu aliikosesha Simba SC bao la kusawazisha dakika ya 88 baada ya kugongesha mwamba wa kulia mkwaju wa penalti kufuatia mshambuliaji Ibrahim Hajib kuangushwa na Nahodha na kiungo Shaaban Nditi.
Refa Michale Magoli aliwatoa kwa kadi nyekundu viungo Mohammed Ibrahim wa Simba na Mohammed Issa wa Mtibwa Sugar dakika ya 86 baada ya kupigana uwanjani.

IMETOLEWA KUTOKA BLOGU YA BIN ZUBEIRY

No comments:

Post a Comment