KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, December 9, 2016

HAYATOU ATUMA RAMBIRAMBI KWA MALINZI KIFO CHA KHALFAN




Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (TFF), Bw. Issa Hayatou ametuma salamu za rambirambi kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Bw. Jamal Emil Malinzi kutokana na kifo cha ghafla cha Mchezaji Ismail Mrisho Khalfan wa timu ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 20 wa Mbao FC ya Mwanza.

“Tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Mchezaji Ismail Mrisho Khalfan akiwa na umri mdogo wa miaka 19 baada ya kuzimia katika mchezo wa Ligi ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 20,” ilisema sehemu ya barua hiyo ya Rais Hayatou kwenda kwa Rais Malinzi.

“Kwa niaba ya Kamati ya Utendaji ya CAF, familia nzima ya mpira wa Afrika na kwa niaba ya jina langu binafsi, tunapenda kupeleka rambirambi zetu kwa familia ya marehemu na familia ya mpira wa miguu katika Tanzania kwa ujumla wake kufuatia kifo hiki ambacho hakikutarajiwa,” ilisisitiza.

Mchezaji Ismail Mrisho Khalfan wa timu ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 20 wa Mbao FC ya Mwanza, kilitokea Desemba 4, 2016 kwenye Uwanja wa Kaitaba, Bukoba mkoani Kagera wakati timu yake ikicheza mchezo huo dhidi ya Mwadui FC ya Shinyanga.

Timu hiyo ya Vijana wa Mbao, kama vilivyo timu nyingine 7 za Ligi kuu ya Vodacom, ilikuwa Kituo cha Bukoba katika Ligi ya vijana ambayo kwa msimu huu imefanyika kwa mara ya kwanza. Timu nyingine Nane zilikuwa kituo cha Dar es Salaam.

Ismail aliyeanguka uwanjani dakika ya 74, alipata huduma ya kwanza uwanjani hapo kwa madaktari waliokuwa uwanjani, lakini baadaye taarifa za kitabibu zilionyesha amefariki dunia.

Kamati ya Tiba ya TFF, bado inaendelea na uchunguzi wa kifo cha mchezaji huyo kabla ya baadaye kutoa taarifa za kamili ya kitatibu kujua hasa chanzo hasa cha kifo cha mchezaji huyo ambaye mwili wake umehifadhiwa kwenye Hospitali ya Mkoa Kagera. Marehemu Ismail Mrisho Khalfan alizikwa Desemba 5, 2016 jijini Mwanza. 

No comments:

Post a Comment