KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, December 19, 2016

U-23 SASA KUITWA KILIMANJARO WARRIORS


TIMU za taifa za vijana chini ya umri wa miaka 23 kwa wanaume na wanawake ambazo hazikuwa na majina hatimaye zimepatiwa majina.
Taarifa ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) leo imesema kwamba kuanzia sasa U-23 ya wanaume itaitwa Kilimanjaro Warriors wakati ya wanawake itaitwa Kilimanjaro Starlets.
Uteuzi wa majina hayo umefanywa na Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) katika kikao chake kilichofanyika juzi (Desemba 17, 2016) mjini Dar es Salaam.
Timu hizo ambazo ni maalumu kwa ajili ya michuano ya Olimpiki zitaanza maandalizi yake Januari mwakani, na wengi wa wachezaji watakaounda timu hizo zinazojiandaa kwa ajili ya michuano ya Olimpiki itakayofanyika Tokyo, Japan mwaka 2020 watatoka katika timu za sasa za wachezaji wenye umri chini ya miaka 20 (U20).
Mechi za mchujo (qualifiers) kwa ajili ya michuano ya Olimpiki ya 2020 zitaanza mapema mwaka 2019.

No comments:

Post a Comment