KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, December 13, 2016

SIMBA YATWAA UBINGWA KOMBE LA U20



SIMBA SC imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi ya Vijana chini ya umri wa miaka 20 Tanzania Bara, baada ya kuifunga Azam FC kwa penalti 5-3 kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 120.

Katika mchezo huo ulifanyika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), timu zote zilionyesha kandanda safi.
 

Simba walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 14 mfungaji Moses Kitandu aliyemalizia pasi ya George Emmanuel, lakini Shaaban Iddi akaisawazishia Azam dakika ya 28.

Said Mohammed akaifungia Azam FC bao lililoelekea kuwa la ushindi dakika ya 57, kabla ya Said Hamisi kuisawazishia Simba dakika ya 83.


Katika dakika 30 za nyongeza baada ya 90 kukamilika kwa sare ya 2-2, si Simba ya kocha Nico Kiondo wala Azam ya kocha Iddi Nassor ‘Cheche’ iliyofanikiwa kuongeza bao.
 

Waliofunga penalti za Simba ni Calvin Faru, Said Hamisi, Mokiwa Perus, Vincent Costa na Moses Kitandu, wakati za Azam zilifungwa na Abbas Kapombe, Rajab Mohammed na Adolph Bitegeko huku ya Said Mohammed ikipanguliwa na kipa Ally Salum.

No comments:

Post a Comment