KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, December 11, 2016

SIMBA, AZAM KUKUTANA FAINALI YA KOMBE LA U20



AZAM FC itakutana na Simba SC katika fainali ya Ligi Kuu ya Vijana chini ya umri wa miaka 20 baada ya usiku wa jana kuitoa Mtibwa Sugar ya Morogoro kwa penalti 4-2 katika mchezo wa Nusu fainali, kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 120.
Matokeo hayo yanaifanya Azam FC U-20, kukata tiketi ya kuchuana na Simba kwenye mchezo wa fainali kesho Jumapili, utakaofanyika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam saa 1.00 usiku.
Kama ilivyokuwa kwa Azam FC U-20, Simba nayo ililazimika kusubiri hadi changamoto ya kupigiana mikwaju ya penalti ili kuitoa Stand United, kufuatia muda wa kawaida wa mchezo na dakika 30 za nyongeza kuisha kwa sare ya bao 1-1 na hivyo wekundu hao kushinda 8-7.

No comments:

Post a Comment