KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, December 26, 2016

SIMBA YAIONYESHA UNDAVA JKT RUVU


SIMBA jana iliendelea kuwapa raha mashabiki wake baada ya kuichapa JKT Ruvu bao 1-0 katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara, iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Bao pekee na la ushindi la Simba lilifungwa na kiunga Muzamil Yassin dakika ya 45 baada ya kaz nzuri iliyofanywa na Pastory Athanas.

Kutokana na ushindi huo, Simba inaendelea kuongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 42 baada ya kucheza mechi 17, ikiwa mbele ya watani wao wa jadi Yanga, kwa tofauti ya pointi nne.

Timu hizo zilikianza kipindi cha kwanza kwa kushambuliana kwa zamu, huku safu za viungo za pande zote mbili zikionyeshana umahiri wa kutawala idara hiyo.

No comments:

Post a Comment