KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, January 17, 2016

SIMBA YAITUNGUA MTIBWA SUGAR BAO 1-0



BAO lililofungwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Hamisi Kiiza, jana liliiwezesha Simba kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar.

Katika mechi hiyo ya ligi kuu ya Tanzania Bara, iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Kiiza alifunga bao hilo dakika ya tano ya mchezo.

Mganda huyo alifunga bao hilo kwa kichwa, akimalizia krosi maridhawa iliyopigwa na Ibrahim Ajib kutoka pembeni ya uwanja.

Kwa ushindi huo, Simba sasa imefikisha pointi 30 baada ya kucheza mechi 14 huku ikiwa nafasi ya tatu, nyuma ya mabingwa watetezi Yanga, wenye pointi 32 na Azam yenye pointi 35.

Katika mechi zingine za ligi hiyo zilizochezwa juzi, Azam ilitoka sare ya bao 1-1 na African Sports, JKT Ruvu ilipata kipigo cha mabao 5-1 kutoka kwa Mgambo Shooting, Mbeya City iliichapa Mwadui bao 1-0, Coastal Union ilitoka sare ya bao 1-1 na Majimaji wakati Prisons iliichapa Toto African bao 1-0.

No comments:

Post a Comment