KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, January 18, 2016

YANGA YAITUNGUA NDANDA UNITED 1-0 NA KUREJEA KILELENI LIGI KUU

MABINGWA watetezi Yanga mwishoni mwa wiki walirejea kileleni mwa ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara baada ya kuichapa Ndanda United bao 1-0.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga ilijipatia bao hilo la pekee kipindi cha kwanza kupitia kwa beki wake Kevin Yondan.

Ushindi huo uliiwezesha Yanga kuwa na pointi 36 sawa na Azam, lakini inaongoza kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.

Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena kesho wakati mabingwa wa zamani Simba watakapomenyana na JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Taifa wakati Azam itavaana na Mgambo JKT kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Katika mechi zingine, Stand United watakuwa wenyeji wa Toto Africans, Mbeya City watakuwa wageni wa Ndanda FC wakati Prisons itavaana na Coastal Union mjini Mbeya.

Yanga wanatarajiwa kushuka tena dimbani keshokutwa wakati Yanga watakapoikaribisha Majimaji kwenye Uwanja wa Taifa,
Mwadui itavaana na Kagera Sugar mjini Shinyanga wakati African Sports itavaana na Kagera Sugar mjini Tanga.

No comments:

Post a Comment