KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, January 21, 2016

SIMBA YAWAPA RAHA MASHABIKI WAKE



NYOTA ya Kocha Jackson Mayanja kutoka Uganda imeendelea kung'ara baada ya kuiwezesha Simba kushinda mechi ya pili mfululizo katika michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara.

Mwishoni mwa wiki iliyopita, Mayanja aliiongoza Simba kwa mara ya kwanza na kuichapa Mtibwa Sugar bao 1-0 katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kama vile haikutosha, Mayanja jana aliiongoza tena Simba kuichapa JKT Ruvu mabao 2-0 kwenye uwanja huo na hivyo kufufua matumaini ya kutwaa ubingwa wa ligi hiyo msimu huu.

Ushindi huo umeiwezesha Simba kushika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo,ikiwa na pointi 33 baada ya kucheza mechi 15.

Simba ilipata bao la kuongoza dakika ya 51 lililofungwa kwa njia ya penalti na mshambuliaji Hamisi Kiiza baada ya Daniel Lyanga kuchezewa madhambi ndani ya eneo la hatari.


Lyanga aliiongezea Simba bao la pili dakika ya 61 kwa kiki kali iliyomshinda kipa Hamisi Seif wa JKT Ruvu.

Katika mechi zingine za ligi hiyo zilizochezwa jana, Prisons iliichapa Coastal Union mabao 2-1 mjini Mbeya, Azam iliicharaza Mgambo JKT mabao 2-1 mjini Tanga.

No comments:

Post a Comment