KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, January 20, 2016

KIGOGO WA FIFA ATEMBELEA WIZARA YA HABARI



Makamu wa Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Bw. Salman Bin Ebrahim Al Khalifa katikati akiongea na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel kulia kuhusiana na maendeleo ya michezo nchini, wa kwanza kushoto ni Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania Bw. Jamali Malinzi.

(Picha na Benjamin Sawe-WHUSM)

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Asia (AFC), na Makamu wa Rais wa FIFA, Sheikh Salman Bin Ebrahim Al Khalifa leo ametembelea wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, ambapo alifanya mazungmzo mafupi na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Elisante Ole Gabriel.

Katika mazugmzo hayo, Sheikh Salman ameielezea Serikali ya Tanzania nia ya FIFA kuendelea  kushirikiana na Serikali na TFF katika kuendeleza programu mbalibali za maendeleo ya mpira hasa wa vijana na wanawake.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara, Profesa Elisante  ameihakikishia FIFA kuwa nia ya Serikali ni kuona mpira unakua nchini na Serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa TFF na FIFA ili kufikia azama hiyo.

Aidha pia ametoa wito kwa AFC kusaidiana na TFF katika masuala ya exchange programmes ili vijana wetu wapate uzoefu wa nje.

Sheikh Salman na ujumbe wake walitembelea ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) wakiwa na Rais wa TFF, Jamal Malinzi, ambapo walikutana na Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine na kujionea shughuli mbalimbali zinazofanya na shirikisho, ikiwemo uwanja wa Karume, na Hostel zilizopo Karume.

Kiongozi huyo wa AFC, aliwasali nchini jana mchana kwa matembezi ya siku mbili chini ya mwenyeji wake Rais wa TFF, Jamal Malinzi na anatarajiwa kuondoka nchini kesho.

No comments:

Post a Comment