KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, January 24, 2016

YANGA YAIFUATA SIMBA 16 BORA KOMBE LA SHIRIKISHO


MABINGWA wa soka Tanzania Bara, Yanga wametinga hatua ya 16 bora ya michuano ya Kombe la Shirikisho, baada ya kuibanjua Friends Rangers mabao 3-0.

Katika mechi hiyo iliyochezwa jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 2-0.

Yanga sasa imeungana na Simba kucheza hatua hiyo, baada ya juzi kuicharaza Burkina Faso mabao 3-0 mjini Morogoro.

Mshambuliaji Simon Msuva alikuwa wa kwanza kuzifumania nyavu dakika ya tano, akimalizia kona iliyochongwa na Issoufou Boubacar.

Dogo huyo aliiongezea Yanga bao la pili dakika ya 23 baada ya kupokea pasi safi ya Paul Nonga, ambaye naye alipewa pande maridhawa na Salum Telela.

Bao la tatu la Yanga lilifungwa kwa kichwa na Matheo Anthony, akimalizia  krosi ya Telela.

No comments:

Post a Comment