KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, January 28, 2016

SIMBA YATISHIA KUGOMEA MECHI YAO NA YANGA


KLABU ya Simba imetishia kugombea mchezo wake wa mzunguko wa 20 wa ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya watani wao wa jadi, Yanga.

Simba imetoa tishio hilo endapo timu ya Azam na zinginezo, zinazoshiriki michuano hiyo, zitabakiwa na mechi za viporo mkononi.

Mchezo wa Simba na Yanga utachezwa katika mzunguko wa pili wa ligi hiyo, Machi mwaka huu. Katika mechi ya mzunguko wa kwanza, iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Simba ilipigwa mweleka wa mabao 2-0.

Tishio hilo la Simba limekuja siku chache baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kuiruhusu Azam kwenda Zambia, kushiriki katika michuano maalumu, huku ikiacha mechi za viporo dhidi ya Prisons na Ndanda.

Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara, alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, TFF na Bodi ya Ligi Kuu zimevunja kanuni ya ligi kuiruhusu Azam kwenda Zanzibar.

Manara alisema Azam imekwenda Zambia kushiriki bonanza na kuacha kuendelea na ligi, hatua ambayo itaathiri timu zingine katika harakati za kutwaa ubingwa msimu huu.

Alisema TFF imevunja kanuni ya 9 ya kuahirisha mechi, ambapo kifungu (a), kinaeleza mchezo unaweza kuahirishwa endapo timu itakuwa na wachezaji kuanzia watano katika kikosi cha timu ya taifa.

Alisema kifungu (b) kinaeleza kuwa ili timu iweze kuahirisha mchezo wake ni lazima iwe na mechi ya kimataifa na taarifa zitolewe ndani ya siku sita kabla ya kushuka dimbani.

Manara alisema TFF haikupaswa kuiruhusu Azam kwenda Zambia kwa kuwa michuano inayokwenda kushiriki haitambuliwi na Shirikisho la Soka Afrika (CAF).

Aidha, alisema sababu zilizotolewa na TFF kwamba Azam inakwenda huko kwa ajili ya kujiandaa na michuano ya Kombe la Shirikisho nazo hazina mantiki.

Manara alisema wataiandikia barua TFF kutaka ratibaya ligi isibadilishwena ikifika mzunguko wa 20 kila timu ishuke dimbani kucheza.

"Isionekane mwingine anacheza mechi ya mzunguko wa 20 huku timu nyingine zikiwa na mechi za viporo, hatutacheza na tutaigomea ligi,"alisema.

No comments:

Post a Comment