KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, January 29, 2016

TFF YAKIRI KUFANYA MADUDU



SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limekiri kufanya madudu kwa kuiruhusu timu ya Azam kwenda Zambia huku Kuu Tanzania Bara ikiwa bado inaendelea.

TFF imeipa ruhusa ya Azam kwenda Zambia kushiriki michuano maalum kama sehemu ya kujiandaa na michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika huku Ligi Kuu Tanzania Bara ikiwa bado inaendelea.


Hatua hiyo imezua tafrani kwa klabu za Ligi Kuu Tanzania Bara, na baadhi ya wadau wa soka wakipinga uamuzi huo huku baadhi ya klabu zikitishia kugomea mechi za Ligi.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Rais wa TFF, Jamal Malinzi amekiri kuwepo kwa udhaifu huo na kusema kuwa kuondoka kwa Azam kumeathiri timu nyingine katika Ligi Kuu Tanzania Bara.

“Naomba radhi kwa klabu zote 15 za Ligi Kuu Tanzania Bara, tunakiri huu ni udhaifu wa kuiruhusu Azam huku ligi ikiwa inaendelea, tunakubali tumefanya makosa na naomba klabu ziwe na utulivu,”alisema Malinzi.

Malinzi alisema kutokana na tukio hilo wanazihakikishia klabu hakutakuwa na mabadiliko yoyote katika ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara na kwamba Azam ndio itakayokuwa na wakati mgumu katika kulipa mechi zake za viporo.

Malinzi alisema Azam italazimika kucheza mechi mbili ndani ya wiki moja tofauti na timu nyingine ambazo zitakuwa zikicheza mechi moja kwa wiki. 


Alisema pia TFF itahakikisha kunakuwa na usawa wa michezo ili kupisha lawama za kupanga matokeo hivyo amezitaka timu kuondoa hofu juu ya jambo hilo.

“Azam ndio itakayoathirika zaidi katika jambo hili na tunaomba isije ikalalamika kwa kuwa hili wamelitaka wenyewe,”alisema.


 Malinzi Rais Malinzi amesema kamwe TFF haitarudia kosa hilo kwa kuipa ruhusa timu nyingine isafi ri huku Ligi ikiwa bado inaendelea. 

Malinzi amezitaka klabu kuzingatia kanuni za Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kufuata sheria zilizowekwa ili kuepusha usumbufu wa kuvuruga ratiba.

No comments:

Post a Comment