KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, January 24, 2016

TIBOROHA ABWAGA MANYANGA YANGA


KATIBU Mkuu wa Yanga SC, Dk. Jonas Tiboroha amejiuzulu na tayari amewasilisha barua kwa Mwenyekiti, Yussuf Mehboob Manji.
Tiboroha amesema kwamba amechukua uamuzi huo ili apate muda zaidi wa kufanya shughuli zake za Uhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
“Mimi ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kitivo cha Elimu ya Viungo (PE), na kwa kuondoka Yanga SC maana yake napata wasaa mzuri wa kumtumikia mwajiri wangu, UDSM,”amesema.
Pamoja na Tiboroha kutozama ndani sana juu ya kujiuzulu kwake, lakini inaelezwa alikuwa hana maelewano na Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya klabu, Isaac Chanji ambaye kwa sasa ndiye mtu anayesikilizwa na kuaminiwa zaidi na Manji.
Tiboroha alipoulizwa kuhusu mahusiano yake na Chanji alisema: “Nilichoandika katika barua yangu ya kujiuzulu ndiyo sababu za msingi, kikubwa ninawapisha watu ambao wanaweza kuiongoza vizuri Yanga SC kuliko mimi,”amesema.
Tiboroha aliingia Yanga SC Desemba mwaka 2014 akichukua nafasi ya Benno Njovu aliyeondolewa kwa tuhuma mbalimbali. Aliingia Yanga SC akitokea Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kama Ofisa Maendelezo ya Ufundi

No comments:

Post a Comment