KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, January 13, 2016

SERIKALI YAMZAWADIA SAMATTA KIWANJA NA MAPESA LUKUKI



SERIKALI imemzawadia nahodha mpya wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars, Mbwana Samatta, kiwanja kwa ajili ya kujenga nyumba, kilichoko Kigamboni, Dar es Salaam.

Mbali na zawadi hiyo ya kiwanja, serikali pia imempa mchezaji huyo fedha taslim, lakini kiwango chake hakikuwekwa wazi.

Hayo yalisemwa jana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, katika hafla iliyofanyika kwenye Hoteli ya Hyyat Regency, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi kadhaa wa serikali.

Baadhi ya viongozi waliohudhuria hafla hiyo ni Waziri wa Habari, Utamaduni,  Sanaa na Michezo, Nape Nnauye na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Profesa Elisante Ole Gabriel.

Uamuzi wa serikali kumpatia Samatta zawadi hiyo, umekuja siku chache baada ya mchezaji huyo kushinda tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani.

Samatta, aliyekuwa akicheza mpira wa kulipwa katika klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, anatarajiwa kujiunga na klabu ya  KRC Genki ya Belgium.

Wakati huo huo, mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana  Samatta jana alipatiwa viza ya kwenda Ubelgiji kujiunga na klabu ya KRC Genk.

Taarifa ya Ubalozi wa Ubelgiji nchini imesema mwanasoka huyo bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani, alifika kwenye ofisi hizo na kupatiwa viza hiyo.

No comments:

Post a Comment