KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, January 22, 2016

YANGA YATAKATA LIGI KUU, YAIBUGIZA MAJIMAJI 5-0


Refa John Fanuel wa Shinyanga akimkabidhi mpira Amissi Tambwe baada ya mechi kwa kufunga hat trick

Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
YANGA SC imerudi tena kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kufuatia ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Majimaji ya Songea jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ushindi huo unaifanya Yanga SC ifikishe pointi 39, sawa na Azam FC wanaorudi nafasi ya pili – na vijana wa kocha Mholanzi, Hans van der Pluijm wanakaa juu kwa wastani mzuri wa mabao.
Mshambuliaji Mrundi Amissi Joselyn Tambwe amefunga mabao matatu leo, wakati Wazimbabwe, kiungo Donald Ngoma na mshambuliaji Thabani Kamusoko wamefunga bao moja kila mmoja.
Katika mchezo huo uliokuwa wa upande mmoja, dalili za Yanga kuwafanya ‘vibaya’ Majimaji zilianza mapema tu dakika ya nne, baada ya Kamusoko kufunga bao la kwanza akimalizia krosi ya kiungo Deus Kaseke.
Baada ya bao hilo, pamoja na Yanga SC kuendelea kuwashambulia Majimaji, lakini hawakufanikiwa kuongeza mabao hadi kipindi cha pili.
Ngoma alifunga bao la pili dakika 47 kabla ya Tambwe kufunga mara tatu mfululizo dakika za 57, 82 na 84 kuunenepesha ushindi wa mabingwa hao watetezi.
Mechi nyingine za Ligi Kuu leo, Mwadui FC imeshinda 2-1 dhidi ya Kagera Sugar Uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga na African Sports imelazimishwa sare ya 0-0 na Mtibwa Sugar Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

CHANZO CHA HABARI: BLOGU YA BINZUBEIRY

No comments:

Post a Comment