KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, January 10, 2016

SAMATTA NAHODHA MPYA TAIFA STARS

KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa, amemteua mshambuliaji Mbwana Samattam kuwa nahodha mpya wa timu hiyo.

Samatta amechukua nafasi ya nahodha wa zamani wa timu hiyo Nadir Haroub 'Cannavaro'.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Mkwasa alisema uteuzi huo umetokana na kazi nzuri iliyofanywa na Samatta, kuitangaza Tanzania kimataifa.

"Samatta anastahili kuwa nahodha wa Taifa Stars kwa sasa, ingewa tumekuwa na nahodha, ambaye anastahili kuendelea,"alisema Mkwasa.

Aliongeza: "Tumeona kitu pekee cha kumlipa mchezaji huyo kutokana na heshima aliyoiletea nchi yetu ni kumpa beji ya unahodha wa Taifa Stars." 

Hata hivyo, Mkwasa amesema Cannavaro ataendelea kuwa nahodha wa timu ya Tanzania, inayoshiriki michuano ya Afrika kwa wachezaji wa ndani, akisaidiwa na John Bocco.

Uteuzi wa Samatta kuwa nahodha wa Taifa Stars, umekuja siku chache baada ya kuibuka mshindi wa tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani.

Alishinda tuzo hiyo baada ya kupata pointi 127, na kuwabwaga mchezaji mwenzake wa TP Mazembe, Robert Muteba Kidiaba aliyepata pointi 88, Baghdad Bounedjah wa Etoile du Sahel ya Tunisia, aliyepata pointi 63.

No comments:

Post a Comment