KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, January 29, 2016

LIGI YA STARTIMES, SDL KUENDELEA LEO


Vita ya kuwania kupanda daraja msimu ujao itaendelea wikiendi hii kwa michezo 12 ya Ligi daraja la kwanza nchini (Startimes League) kuchezwa katika viwanja mbalimbali kwa makundi A, B, C, kwa kila timu kusaka pointi tatu muhimu.

Jumamosi uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma, wenyeji Polisi Dodoma watakua wenyeji wa Africa Lyon, Kiluvya United wakiwakaribisha Mji Mkuu (CDA) katika uwanja wa Mabatini Mlandizi, Polisi Morogoro dhidi ya Kimondo FC uwanja wa Jamhuri, huku Kurugenzi ikiwakaribisha Burkinafaso kwenye uwanja wa Wambi mjini Mafinga.

JKT Mlale watawakaribisha Njombe Mji uwanja wa Majimaji mjini Songea, Panone dhidi ya Mbao FC uwanja wa Ushirikia Moshi, Polisi Mara watakua wenyeji wa Rhino Rangers uwanja wa Karume mjini Musoma, huku JKT Oljoro wakiwaribisha JKT Kanembwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Ligi hiyo ya StarTimes itaendelea siku ya Jumapili kwa michezo minne kuchezwa, Friends Rangers watakua wenyeji wa Ashanti United uwanja wa Karume, Polisi Dar dhidi ya KMC uwanja wa Mabatini Mlandizi, Lipuli wakicheza dhidi ya Ruvu Shooting uwanja wa Wambi Mafinga huku Polisi Tabora wakicheza dhidi ya Geita Gold uwanja wa Ali Hassani Mwinyi mjini Tabora.
 

Wakati  huo huo, ligi Daraja la Pili nchini (SDL) mzunguko wa pili unatarajiwa kuendelea wikiendi hii kwa michezo 12 kuchezwa katika viwanja mbalimbali nchini, kwa timu nne za juu kutoka makundi A, B, C na D kusaka kupanda daraja msimu ujao.

Kundi A, michezo mitatu itachezwa ambapo Green Warriors watacheza dhidi ya Mvuvuma, Abajalo watawakaribisha Mirambo FC uwanja wa Ali Hassani Miwnyi Tabora, huku Transit Camp wakicheza dhidi ya Singida United uwanja wa Kambarage siku ya Jumapili.

Kundi B, Madini FC watakua wenyeji wa Alliance FC uwanja wa Mbulu, AFC Arusha watacheza dhidi ya Pamba uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha siku ya Jumapili, huku Bulyanhulu FC wakiwakaribisha JKT Rwamkoma siku ya Jumatatu uwanja wa Kambarage Shinyanga.

Kundi C, Leo Ijumaa Cosmopolitan watacheza dhidi ya Kariakoo uwanja wa Karume, Changanyikeni dhidi ya Mshikamano uwanja wa Karume siku ya Jumatatu, huku Abajalo wakicheza dhidi ya Villa Squad siku ya Jumanne.

Kundi D, Jumamosi Mbeya Warriors watacheza dhidi ya Sabasaba uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, Mighty Elephant watacheza dhidi ya Mkamba Rangers siku ya Jumapili uwanja wa Majimaji mjini Songea, huku African Wanderes wakiwakaribisha Wenda FC uwanja wa Wambi Mafinga siku ya Jumatatu.

No comments:

Post a Comment