KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, January 15, 2013

TAMASHA LA MA-STAR WA FILAMU JAN 26

SHIRIKISHO la Filamu Tanzania (TAFF) kwa kushirikiana na wanachama wake, limeandaa onyesho maalum litakalojulikana kwa jina la siku ya 'Ma-Star wa Filamu', linalotarajiwa kufanyika Januari 26, mwaka huu katika ukumbi wa Dar Live Mbagala, Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa TAFF, Simon Mwakifwamba alisema, onyesho hilo ni maalum kwa ajili ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kujenga ofisi ya shirikisho hilo na kunua vitendea kazi muhimu vya ofisi.

"Katika moja ya changamoto za uendeshaji wa TAFF ni kutokuwa na ofisi pamoja na vitendea kazi muhimu ndani ya ofisi. Vifaa hivyo ni kama vile kompyuta, kabati za kuhifadhia nyaraka, mashine ya kudurufu nyaraka, viti na meza za watendaji," alisema Mwakifwamba.

Aliongeza kuwa, fedha zinazohitajika kwa ajili ya kazi hiyo ni sh.milioni 60, hivyo kwa kupitia onyesho hilo, wana uhakika wa kupata kiasi hicho cha pesa.

Mwakifwambva alisema onyesho hilo limepangwa kuanza saa sita mchana kwa burudani za watoto, ambazo zitadumu hadi saa 12 jioni na kiingilio kitakuwa sh.2,000.

Alisema burudani kwa ajili ya watu wazima zitaanza saa mbili usiku kwa kiingilio cha sh. 15,000 kwa viti vya VIP na sh. 7,000 kwa viti vya kawaida.

Alizitaja burudani zitakazokuwepo katika onyesho hilo kuwa ni pamoja na muziki kutoka kwa wasanii wa filamu wanaojihusisha na fani hiyo, kundi la Shilole Classic na vichekesho vya King Majuto, Kitale, Kingwendu, Snura na kundi lake, Hemed PHD, Masanja Mkandamizaji na Alex wa Michejo.

Aliwataja wasanii wengine wanaotarajiwa kutoa burudani katika onyesho hilo kuwa ni Jackline Wolper, Irene Uwoya, Aunt Ezekiel, JB, Rich Rich, Ray, Steve Nyerere na washereheshaji Ben Kinyaiya na Chiki Mchoma.

Kwa mujibu wa Mwakifwamba, onyesho hilo limedhaminiwa na kampuni za Baucha Records, Clouds Midia, Global Publishers, ASET, Times FM, Steps Entertainment na VANNEDRICK Tanzania ltd.

No comments:

Post a Comment