KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, January 15, 2013

TFF KUITAFUTIA STARS MECHI NGUMU

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limesema lipo katika mchakato wa kuitafutia mechi ya kirafiki ya kimataifa timu ya Taifa, 'Taifa Stars'.

Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, mchezo huo unaweza kufanyika Februari 6 mwaka huu, ikiwa ni tarehe iliyopangwa na Shirikisho la Kimataifa la Soka (FIFA) kwa mechi za kirafiki.

Wambura alisema lengo la mechi hiyo ni kuipa mazoezi Taifa Stars kwa ajili ya kujiandaa kwa mechi yake ya michuano ya kuwania kucheza fainali za Kombe la Dunia za 2014 dhidi ya Morocco.

Taifa Stars na Morocco zimepangwa kumenyana Machi 22 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Wambura alisema lengo la TFF ni kutafuta timu yenye kiwango cha juu ili kuipa Taifa Stars mazoezi ya kiwango cha juu na kuwafanya wachezaji wajiamini.

Alisema Morocco ni timu nzuri na ambayo inashiriki katika fainali za mwaka huu za Mataifa ya Afrika, hivyo ni vyema Taifa Stars ikapata kipimo kizuri kabla ya kuwakabili wapinzani wao.

Tayari Taifa Stars imeshacheza mechi mbili za kirafiki hadi sasa. Katika mechi ya kwanza, iliichapa Zambia bao 1-0 kabla ya kufungwa mabao 2-1 na Ethiopia mjini Addis Ababa.

No comments:

Post a Comment