KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, January 27, 2013

SIMBA, LYON ZAINGIZA MIL 53/-



MCHEZO wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, uliozikutanisha timu za Simba na African Lyon umeingiza sh. 53,756,000.

Katika mchezo huo uliofanyika katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, jumla ya watazamaji 9,408 walikata tiketi na kushuhudia mchezo huo, ambapo Simba ilishinda mabao 3-1.

Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura, alisema jana kuwa, kutokana na mapato hayo kila klabu ilipata mgawo wa sh. 12,499,752.45.

Wambura alisema mgawo mwingine ulikuwa wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), iliyolipwa sh. 8,200,067.80, wakati asilimia 15 ya uwanja ni sh.6,355,806.33.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni gharama za tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 3,813,483.80, Kamati ya Ligi sh. 3,813,483.80, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF), sh. 1,906,741.90 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,483,021.48.

Viingilio katika mchezo huo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.

No comments:

Post a Comment