KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, January 19, 2013

WALANGUZI WA TIKETI ZA MPIRA BYE BYE

ASILIMIA 80 ya maandalizi ya kutumika kwa mfumo mpya wa tiketi za elektroniki utakaoanza kutumika hivi karibuni katika michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara imekamilika.

Hayo yalisemwa mjini Dar es Salaam jana na Mkurugenzi wa Takwimu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Saad Kawemba alipokuwa akizungumzia maendeleo ya ufungwaji wa mashine mpya za kuuza tiketi hizo.

Kawemba alisema asilimia iliyobaki ni kwa ajili ya ufungwaji wa mashine hizo. Alisema ufungwaji wa mashine hizo utakamilika baada ya kuwasili kwake.

Ufungwaji wa mashine hizo unasimamiwa na Benki ya CRDB, ambayo ilishinda tenda ya kufanya kazi hiyo. Kawemba alisema mashine hizo zitafungwa katika viwanja vinane vinavyotumika katika mechi za ligi hiyo.

Alivitaja viwanja hivyo kuwa ni Kaitaba wa Kagera, CCM Kirumba wa Mwanza, Sheikh Amri Abeid wa Arusha, Mkwawani wa Tanga, Sokoine wa Mbeya, Jamhuri wa Dodoma na Taifa wa Dar es Salaam.

Alisema baada ya kufungwa kwa mashine hizo, hakutakuwa na mtu atakayenunua tiketi barabarani katika katika magari maalumu kama ilivyo sasa.

Kawemba alisema mfumo huo mpya utamuwezesha mtu atakayehitaji tiketi, kuzinunua kupitia katika ATM za benki ya CRDB, M-PESA, Tigopesa na Airtel Money.

Alisema baada ya kununua tiketi, mmiliki wake atakwenda kuichapicha katika mashine hizo, ambazo zitawekwa katika sehemu maalum na kisha kwenda nayo uwanjani, ambapo tiketi hiyo ndiyo itakayomfungulia mlango wa kuingia uwanjani.

No comments:

Post a Comment