KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, January 24, 2013

FLAVIANA AWA MWANAMITINDO BORA AFRIKA 2012



MREMBO na mwanamitindo nyota wa Tanzania, Flaviana Matata ameendelea kung’ara kimataifa baada ya kushinda tuzo ya 'Nigeria’s Next Super Model'.

Flaviana alishinda tuzo hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Lagos, Nigeria na kuwa mwanamitindo bora wa Afrika 2012 (Africa’s Most Outstanding Model 2012).

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Compass Communication Tanzania Limited, Maria Sarungi Tsehai alisema jana kuwa, ushindi huo wa Flaviana ni sifa na changamoto kwa wanamitindo wa Tanzania wanaochipukia.

Maria alisema amejisikia faraja kubwa kutokana na mafanikio hayo ya Flaviana kwa sababu yeye ndiye aliyemvumbua mwanamitindo huyo, ambaye kwa sasa anashika chati ya juu nje ya nchi.

Aliongeza kuwa, Flaviana amedhihirisha ubora wake na mpaka sasa kiwango chake cha kuitangaza Tanzania kimataifa ni ndoto aliyokuwa nayo kwa muda mrefu.

Tuzo aliyopata mwanamitindo huyo hutolewa kwa wanamitindo, ambao bado wanailetea sifa Afrika kimataifa. Flaviana amekuwa katika chati ya juu, ambapo Desemba mwaka jana, alishinda tuzo ya mwanamitindo bora kutoka kwa diaspora ya Waafrika.

Flaviana kwa sasa anaishi na kufanya kazi ya uanamitindo mjini New York nchini Marekani kupitia shirika la Wilhelmina Models.

Mwanamitindo huyo pia anaendesha taasisi yake, inayojulikana kwa jina la Flaviana Matata Foundation, ambayo inasomesha watoto yatima wa kike 16 nchini.

No comments:

Post a Comment