KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, January 25, 2013

SERIKALI YAPUNGUZA MAKATO U/TAIFA, TRA KUREJESHA FEDHA ZA TFF



SERIKALI imekubali kupunguza makato mbalimbali yanayotolewa wakati wa mechi za michuano ya soka ya ligi kuu ya Tanzania Bara na Kimataifa.


Uamuzi huo umetangazwa leo na Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla alipokuzungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam.

Makalla alisema kuanzia sasa, serikali itakuwa ikichukua asilimia 15 ya mapato yanayopatikana katika mechi hizo, hasa zinazochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ili kuzipunguzia gharama klabu.

Alisema baada ya serikali kupata asilimia hiyo ya mapato, hakutakuwa na asilimia zingine zitakazokatwa zaidi ya gharama za tiketi.

Aliwashuru viongozi wa klabu, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na waandishi wa habari kwa kusimama kidete kulisimamia jambo hilo kwa vile ni kweli klabu zilikuwa zikiachiwa mzigo mkubwa wa gharama.

Makalla alisema pia kuwa, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekubali kurejesha fedha ilizochokua kutoka kwenye akaunti ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa ajili ya nauli za klabu.

Fedha hizo, sh. milioni 150 zilitolewa na wadhamini wa ligi kuu ya Tanzania Bara, Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom kwa ajili ya nauli kwa timu zinazoshiriki mzunguko wa pili wa ligi hiyo.

Awali, klabu za ligi hiyo pamoja na kamati ya ligi, zilitishia kususia kucheza mechi za mzunguko huo iwapo TRA isingerejesha fedha hizo.

Hata hivyo, Makalla amezitaka klabu kuwa na subira kwa vile utaratibu wa kurejesha fedha hizo hauwezi kufanyika kwa siku moja. Alisema utaratibu huo unaweza kuchukua muda kidogo, lakini lazima fedha hizo zirejeshwe.

No comments:

Post a Comment