KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, January 27, 2013

MALINZI, NYAMLANI, MANJI WAWEKEWA PINGAMIZI TFF



WAGOMBEA wa nafasi ya urais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Athumani Nyamlani na Jamal Malinzi, wamewekewa pingamizi la kugombea nafasi hiyo.

Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, Nyamlani amewekewa pingamizi mbili na Mtanga Yussuf na Menard Justine wakati Malinzi amewekewa pingamizi moja na Agape Fuwe.

Angetile alisema kamati ya uchaguzi imepokea pingamizi 14 za wagombea wanaowania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi mkuu wa TFF unaotarajiwa kufanyika Februari 24 mwaka huu.

Aliwataja wagombea wengine waliowekewa pingamizi kuwa ni Michael Wambura, anayewania nafasi ya makamu wa rais, ambaye amewekewa pingamizi mbili na Osiah Samuel na Saidi Rubeya.

Kwa mujibu wa Angetile, wagombea wa nafasi ya ujumbe wa kamati ya utendaji waliowekewa pingamizi ni Epatha Swai, aliyewekewa pingamizi mbili na Ramadhan Sesso na Sos Chalamila, Eliud Mvella amepingwa na Saidi Kiponza, Abdul Changawa na Peter Namengi wakati Athumani Kambi amepingwa na Jeremiah Wambura.

Kwa upande wa Bodi ya Ligi, Angetile alisema wagombea wa nafasi ya mwenyekiti, Yussuf Manji na Ahmad Yahya wamewekewa pingamizi mbili kila mmoja.

Alisema Manji amewekewa pingamizi na mwanachama maarufu wa Simba, Daniel Kamna na mwanachama wa Yanga, Juma Magoma wakati Yahya amewekewa pingamizi na Frank Mchaki na Mohamed Saidi.

Angetile alisema kamati ya uchaguzi ya TFF inatarajiwa kukutana keshokutwa kujadili pingamizi hizo kabla ya kutangaza majina ya wagombea, watakaopitishwa katika uchaguzi huo.

No comments:

Post a Comment