KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, July 4, 2013

KHADIJA MNOGA, PAULYNE ZONGO WAUNGANA



WANAMUZIKI nyota watatu wa kike nchini wameanzisha kundi jipya la muziki litakalojulikana kwa jina la Ndege Watatu.

Nyota hao watatu wanaongozwa na Khadija Mnoga, ambaye ni mwimbaji wa bendi ya Extra Bongo, Paulyne Zongo na Joan Matovolwa, ambao ni wanamuziki huru.

Khadija alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, tayari kundi hilo limesharekodi kibao kimoja kinachokwenda kwa jina la Misukosuko ya Mapenzi.

Kwa mujibu wa Khadija, tayari kibao hicho kimeshaanza kurushwa katika vituo mbalimbali vya redio nchini na kupokewa vizuri na mashabiki.

Alisema kibao hicho kimetungwa kwa pamoja na wanamuziki hao watatu kwa kiwango cha juu kwa lengo la kuonyesha umahiri wao katika muziki.

Khadija alisema kundi hilo linaundwa na wanamuziki mchanganyiko wa miondoko ya dansi na kizazi kipya na limedhamiria kuleta ladha na changamoto mpya katika muziki.

No comments:

Post a Comment