KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, July 22, 2013

SIMBA, YANGA DIMBANI OKTOBA 20 LIGI KUU YA BARA


HATIMAYE Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetangaza ratiba ya michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2013/2014, ambayo inaonyesha kuwa, timu kongwe za Simba na Yanga zitakutana Oktoba 20 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ratiba hiyo iliyotolewa leo inaonyesha kuwa, mechi ya kuwania Ngao ya Jamii kati ya mabingwa, Yanga na washindi wa pili msimu uliopita, Azam itapigwa Agosti 17 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa ratiba, ligi hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Agosti 24 mwaka huu kwa timu zote 14 kushuka dimbani katika miji saba tofauti.

Katika mechi hizo za ufunguzi,  Yanga itacheza na Ashanti United (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam), Mtibwa Sugar na Azam (Uwanja wa Manungu, Morogoro) na JKT Oljoro na Coastal Union (Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha).

Nyingine ni Mgambo Shooting na JKT Ruvu (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga), Rhino Rangers na Simba (Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora), Mbeya City na Kagera Sugar (Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, Mbeya), na Ruvu Shooting na Tanzania Prisons (Uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Pwani).

Mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo utamalizika Novemba 3 mwaka huu wakati wa pili utamalizika Aprili 27 mwakani. (Ratiba ya mzunguko wa kwanza na wa pili imeambatanishwa- attached).

No comments:

Post a Comment