KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, July 25, 2013

KIOTA KIPYA CHA MARAHA CHA SERENGETI GOLDEN PARADISE, MBANDE, MBAGALA, DAR ES SALAAM

 

Hoteli ya Serengeti Golden Paradise Resort  imeleta mapinduzi makubwa katika kutoa huduma za hoteli na burudani ya muziki katika maeneo ya Mbande, Mbagala, ambayo yako pembezoni mwa jiji la Dar es Salaam.

Licha ya ukumbi wa hoteli hiyo kuwa wa kisasa na wenye uwezo wa kuchukua mashabiki wengi kwa wakati mmoja, unaweza kuonekana mdogo kutokana na kujitokeza kwa umati mkubwa wa watu wakati wa maonyesho mbalimbali.
Meneja wa hoteli hiyo, Wambura Sungura anasema kuzinduliwa kwa ukumbi huo kumeleta faraja kubwa kwa wakazi wa Mbagala na vitongoji vyake kutokana na kupata huduma, ambazo wamekuwa wakizikosa na badala yake kulazimika kusafiri kwenda mbali kuzitafuta.

“Kwa sasa ni kama kuunga mkono mpango wa serikali wa kuhakikisha huduma zote muhimu kama hizi za hoteli zinapatikana nje ya miji ili kupunguza kila kitu watu wakifate mjini, matokeo yake kusababisha msongamano mjini bila sababu za msingi,”anasema.
“Pia siku hizi watu hawataki bugudha mijini, badala yake wanataka kwenda sehemu tulivu na zenye hadhi kama hizi kwa kupumzika baada ya shughuli za wiki nzima, hali inayowafanya watafute sehemu nzuri za kupumzika na sehemu za namna hii ni nzuri kwao,”anasema Sungura.

Meneja huyo anasema wameandaa utaratibu wa kuvialika vikundi mbalimbali vya burudani kila mwisho wa wiki ili kutoa fursa kwa wakazi wa Mbagala na vitongoji vyake kutohangaika kusafiri umbali mrefu kwenda mjini au maeneo mengine kutafuta burudani.

“Tunataka watu wasiwe wanahangaika kutoka hapa kutafuta burudani, tutajitahidi kuhakikisha kuwa kila wasanii wanaopendwa na wateja tunawaleta ili kukoga nyoyo zao,”anasema.

Anaongeza kuwa, kwa sasa wanatoa huduma mbalimbali ikiwemo malazi, vinywaji na chakula, kitu ambacho kama  mteja akifika hapo hawezi kujutia nafsi yake, badala yake atakuwa anatamani kwenda kupata huduma mara kwa mara.
Anasema pamoja na kufungua hoteli hiyo, wanashiriana na wateja kupata maoni yao juu ya namna bora ya kuboresha huduma ili kuleta mageuzi makubwa katika kutoa huduma bora zaidi.

No comments:

Post a Comment