KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, July 24, 2013

OMOTOLA APINGA NDOA ZA UTOTONI



LAGOS, Nigeria
MWANAMAMA nyota katika uigizaji wa filamu wa Nollywood, Omotola Jalade ametaka kusiwepo kipengele kinachoruhusu ndoa za utotoni kwenye katiba ya nchi hiyo.
Akizungumza wakati wa shindano la urembo la MBGN lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita mjini hapa, Omotola alisema anapinga ndoa hizo za utotoni kwa watoto wa kike.
Omotola ameelezea msimamo wake huo wakati ambapo serikali ya nchi hiyo iko katika mchakato wa kuifanyia marekebisho katiba ya nchi hiyo.
Mwanadada huyo amewataka maseneta wa Nigeria kutopiga kura za kuunga mkono kipengele kinachohusu ndoa hizo.
Omotola alisema atashangaa iwapo maseneta wa Nigeria hawatapitisha sheria, itakayohakikisha kwamba, kila mtoto anakuwa na haki ya kwenda shule kupata elimu.
"Idadi kubwa ya watoto hivi sasa wapo mitaani wakiomba, kunyanyaswa na kubakwa ama kuolewa na wanaume, ambao wanapaswa kuwalinda. Nani anayewalinda watoto wa Nigeria? Je, tusubiri Milala kabla ya kuchukua hatua? Je, tunapaswa kuondoa tangazo la tahadhari kwenye filamu zetu linalosema, 'Haipaswi kutazamwa na watoto wa chini ya miaka 18?" Alihoji.
Mwanamama huyo mwenye watoto wanne ametaka watoto wa kike wa Nigeria wawe na haki ya kupata elimu, kufurahia maisha ya utoto na kuwa na uamuzi juu ya nani anayepaswa kufunga naye ndoa na lini.
"Napinga ndoa za utotoni na mswada wa baraza la seneti unaotaka kuidhinishwa kwa ndoa hizo Nigeria,"alisema.

No comments:

Post a Comment