KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, July 21, 2013

YANGA CHUPUCHUPU KWA URA



Wachezaji wa URA wakishangilia bao lao la pili dhidi ya Yanga leo.
Wachezaji wa Yanga wakishangilia baada ya Jerry Tegete kusawazisha dakika ya 90. (Picha zote kwa hisani ya Habari Mseto)

BAO lililofungwa na mshambuliaji Jerry Tegete dakika ya 90 leo limeinusuru Yanga kuadhiriwa na URA ya Uganda baada ya timu hizo kutoka sare ya bao 2-2 katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mechi hiyo iliyokuwa na ushindani mkali, Yanga ilikwenda mapumziko ikiwa nyuma kwa bao 1-0. Bao hilo la kuongoza lilifungwa na Litumba Yayo dakika ya 42.

Litumba ndiye aliyeizamisha Simba katika mechi ya jana baada ya kuifungia URA mabao yote mawili ilipoibuka na ushindi wa mabao 2-1.

Bao la pili la URA lilifungwa tena na Litumba dakika ya 61 kwa shuti kali la mpira wa adhabu lililowapita mabeki wa Yanga na kipa Deogratius Munishi 'Dida' aliyejaribu kuupangua mpira, lakini ulimshinda nguvu.

Mrundi, Didier Kavumbagu aliifungia Yanga bao la kwanza dakika ya 66 alipounganisha wavuni kwa kichwa krosi maridadi iliyopigwa na Juma Abdul kutoka pembeni ya uwanja.

Tegete aliisawazishia Yanga baada ya kuwazidi nguvu na mbio mabeki wawili wa URA pamoja na kipa wao, Yassin Mugabi.

Mrundi Didier Kavumbangu alianza dakika ya 66 akiunganisha krosi ya beki Juma Abdul kabla ya Tegete kusawazisha dakika ya 90 baada ya kuwazidi nguvu na maarifa kipa wa URA, Yassin Mugabi na mabeki wawili.

No comments:

Post a Comment