KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, July 24, 2013

GENEVIENE ANASA KIMAPENZI KWA MENSAH



LAGOS, Nigeria

MCHEZA filamu nyota wa kike wa Nigeria, Gevenieve Nnaji huenda akafunga ndoa na mfanyabiashara wa Ghana, Mathew Mensah.

Genevieve na Mensah wamekuwa wakionekana pamoja mara kwa mara na baadhi ya watu walio karibu nao wameeleza kuwa, wapo katika mapenzi mazito.

Marafiki wa Genevieve wameeleza kuwa, mwanadada huyo, ambaye ni mama wa mtoto mmoja, anaonekana kulifurahia penzi hilo.

Awali, Genevieve alikuwa akihusishwa kimapenzi na mwanamuziki D'banj, lakini wote wawili walikuwa wakizikana taarifa hizo na kudai kuwa, uhusiano wao ulikuwa wa kawaida.

Alipoulizwa na rafiki zake kuhusu uhusiano uliopo kati yake na Mensah, Genevieve alidai kuwa ni wa kawaida, lakini wadadisi wa mambo wanahisi kuwa, kuna kitu kingine zaidi kinachoendelea kati yao.

Kwa mujibu wa marafiki hao wa Genevieve, mwanadada huyo amekuwa akilitaja mara kwa mara jina la Mensah katika mazungumzo yake ya kila siku.

Mensah ni miongoni mwa marafiki wa Genevieve waliohudhuria sherehe ya mcheza filamu huyo kufikisha umri wa miaka 33 iliyofanyika hivi karibuni mjini Lagos.

"Upo uwezekano mkubwa kwa Genevieve kufunga ndoa na Mensah kabla ya mwisho wa mwaka huu. Inawezekana ikawa Desemba," kilisema chanzo cha habari.

Wakati huo huo, Genevieve hivi karibuni alionekana akiwa mjini Beijing, China alikokwenda kwa ziara maalumu.

Mwanadada huyo mwenye mvuto, aliyecheza filamu zaidi ya 80 za Kinigeria, alionekana akitembelea madumba mbalimbali yanayouza majani ya chai na viwanda vya nguo.

No comments:

Post a Comment