KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, July 11, 2013

M2 THE P KUCHORA SURA YA MANGWEA MGONGONI KWAKE


MSANII  wa muziki wa kizazi kipya, M2 The P amesema atachora tattoo kubwa yenye sura ya marehemu Albert Mangweha kwenye mgongo wake.
M2 The P alisema wiki hii mjini Dar es Salaam kuwa, amefikia uamuzi huo kwa lengo la kumkumbuka na kumuenzi rafiki yake huyo, aliyefariki dunia hivi karibuni nchini Afrika Kusini na kuzikwa Morogoro.
Msanii huyo alikuwa pamoja na Mangweha nchini Afrika Kusini kabla na siku ya kifo chake.
Alisema kabla ya kifo cha Mangweha, alimwelezea kuhusu sababu zilizomfanya achore tattoo ya chozi na ya muziki kwenye mikono yake yote miwili.
Akifafanua, alisema tattoo ya chozi ililenga kumuenzi mama yake mzazi na ile ya muziki inaonyesha jinsi fani hiyo ilivyo kwenye damu yake.
"Sasa nataka kuchora tattoo kubwa mgongoni yenye picha yake. Nadhani ndio itakuwa kumbukumbu yangu kubwa kwake. Nitakichora kichwa cha Albert Mangweha,"alisema.
M2 The P alisema anamshukuru Mungu kwamba kwa sasa anarejea katika hali yake ya kawaida baada ya kuondokewa na kipenzi chake huyo, waliyesafiri pamoja kwenda Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment