KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, July 24, 2013

OGE OGOYE ASHUSHA GHOROFA



LAGOS, Nigeria
MWANADADA Oge Okoye amedhihirisha kwamba filamu zinalipa baada ya kushusha mjengo wa ghorofa katika moja ya mitaa ya Jiji la Lagos.
Mwigizaji huyo machachari wa Nigeria sasa ameamua kula 'kuku kwa mrija' baada ya kuitumikia fani hiyo kwa miaka mingi na kwa mafanikio makubwa.
Oge, ambaye amekuwa akicheza filamu kwa zaidi ya muongo mmoja sasa, ameshusha mjengo huo kwa kutumia mamilioni ya naira za Nigeria.
Hata hivyo, bado ujenzi wa ghorofa hilo haujakamilika, lakini tayari kumeshawekwa mageti ya vyuma.
Baadhi ya wadau wa fani ya filamu nchini Nigeria, wamempongeza mwanadada huyo kwa uamuzi wake huo wa kujenga nyumba hiyo ya  ghorofa kwa vile waigizaji wenzake wengi wameshindwa kufikia hatua hiyo.
Kwa mujibu wa wadau hao, wacheza filamu wengi wa nchi hiyo wamekuwa wakiishi nyumba za kupanga na kuishia kununua magari ya kifahari.

No comments:

Post a Comment