KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, March 1, 2015

AZAM YATUPWA NJE KOMBE LA AFRIKA

WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano ya soka ya klabu bingwa Afrika, Azam jana waliyaaga mashindano hayo baada ya kuchapwa mabao 3-0.

Katika mechi hiyo iliyochezwa mjini Khartoum, Azam ilikuwa ikihitaji sare ya aina yoyote ili iweze kusonga mbele.

Kutokana na kipigo hicho, Azaam imetolewa kwa jumla ya mabao 3-2 kufuatia kushinda mechi ya awali mjini Dar es Salaam kwa mabao 2-0.

Dalili za Azam kutolewa katika michuano hiyo zilianza kujionyesha mapema kutokana na waamuzi wa mchezo huo kutoka Zambia kuwapendelea wenyeji.


Katika kudhihirisha upendeleo wa dhahiri, wenyeji walizawadiwa penalti kipindi cha kwanza, lakini iliokolewa na kipa Aishi Manula.

No comments:

Post a Comment